Home KITAIFA WAZIRI MKUU ALIA NA JAMII MMOMONYOKO WA MAADILI

WAZIRI MKUU ALIA NA JAMII MMOMONYOKO WA MAADILI

 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa wito kwa jamii kuwa walinzi wa watoto na kujijengea utamaduni wa kutoa taarifa vinapotokea vitendo vya ukiukwaji wa maadili.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya mtoko na mama ambapo amesisitiza maadili ndio utambulisho wa kila mmoja katika jamii.

“Watanzania wote tushirikiane kukemea vikali vitendo vyote vya mmomonyoko wa maadili kwa kisingizio chochote,Mkataa kwao ni Mtumwa, sisi ni watu huru” amesema Waziri Mkuu Majaliwa

Aidha amewasihi Viongozi wa madhehebu ya dini kuendelea kuwalea watoto kiroho na kuwahimiza kuacha vitendo visivyofaa kwa kuwa havimpendezi Mwenyezi Mungu.

Previous articleMWENYEKITI WA UVCCM MWANZA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MAGU
Next articleSERIKALI KUPITIA TANROADS YASAINI MIKATABA MIWILI YA MIRADI YA KIMAKAKATI MKOANI SINGIDA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here