Home KITAIFA WANAFUNZI TUMIENI MICHEZO KUJIFUNZA UZALENDO

WANAFUNZI TUMIENI MICHEZO KUJIFUNZA UZALENDO

NA DENIS SINKONDWE, SONGWE.

MKUU wa wilaya ya Ileje mkoani Songwe Mhe.Farida Mgomi amewahimiza wanafunzi wa shule za msingi mkoani humo kushiriki mashindano ya michezo mbalimbali Kwa lengo la kujifunza uzalendo.

Mhe. Mgomi amesema hayo Mei 19,2023 akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Songwe Mhe Dr Francis Michael wakati akifunga mashindano ya UMITASHUMTA ngazi Ya mkoa kwenye viwanja vya shule ya sekondari Ileje.

Mhe. Mgomi amesema michezo inasaidia kuimarisha mwili, kujenga afya ya akili, uzalendo wa nchi hali ambayo inawasidia vijana kujiajili na kuwaingizia kipato.

“Nawasihi wanangu jihusisheni na michezo kwani mtajifunza kanuni bora sambamba na kuwajengea upendo baina ya wanamichezo”,amesema Mhe. Mgomi

Akimwakilisha Afisa elimu mkoa wa Songwe Michael Ligola ,afisa utamaduni wa mkoa huo Godfrey Msokwa amesema mashindano hayo ngazi ya mkoa yalijumuisha wanamichezo 537 huku michezo ya wanawake imekua Kwa Kasi.

Msokwa ametaja idadi ya wanamichezo Kila halmashauri kuwa Ileje 139, Mbozi 120, Momba 82, Songwe 95 na Tunduma 120.

Katika mashindano hayo wilaya ya Mbozi imeibuka mshindi wa jumla kati ya michezo yote iliyochezwa .

Previous articleMKATABA WA MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA LABAY-HAYDOM (KM 25) WASAINIWA
Next articleOTHMAN KUONGOZA TIMU YA ACT MAGEUZI YA KISIASA ZANZIBAR

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here