Home SIASA UWT MKOA WA SONGWE YATEMBELEA SHULE ILIYOUNGUA BWENI

UWT MKOA WA SONGWE YATEMBELEA SHULE ILIYOUNGUA BWENI

 

NA DENIS SINKONDE, SONGWE

Jumuiya ya umoja wa wanawake Tanzania CCM mkoa wa Songwe imetembelea shule ya sekondari Vwawa na kutoa vitu mbalimbali Kwa wanafunzi baada ya bweni la wanafunzi kuungua Kwa moto hivi karibuni.

Jumuiya hiyo imeongozwa na mwenyekiti wake Emelia Mwakyoma Aprili 20,2023.

Mwakyoma kwaniaba ya jumuiya amekabidhi mashuka, Sabuni na nguo za ndani Kwa wanafunzi hao lengo likiwa ni kuwafariji baada ya vitu vyao kuteketea Kwa moto.

Baada ya kukabidhi vifaa hivyo Mwakyoma amewasihi wadau wengine kuendelea kujitolea kutoa msaada kuwapa wanafunzi Ili wasiwe na hofu ya mahitaji katika kipindi ambacho wanafunzi hao ambao wapo kidato Cha sita wataanza mitihani ya kitaifa ya kuhitimu

Mwakyoma ameongeza Kwa kuawaasa wanafunzi hao waendelee kuamini kuwa watafauru mitihani yao kwani Mungu yu pamoja na watarajie walichokisoma na kukielewa ndicho kinaenda kutokea kwenye mitihani yao.

Previous articleWIKI YA UBUNIFU KUFANYIKA DODOMA
Next article“SERIKALI IMESAJILI MIRADI YA UWEKEZAJI 537″_WAZIRI MAJALIWA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here