Home KITAIFA PWANI YAADHIMISHA SIKU YA USHAIRI WA WATOTO DUNIANI (WoChiPoDa)

PWANI YAADHIMISHA SIKU YA USHAIRI WA WATOTO DUNIANI (WoChiPoDa)

Mratibu wa WoChiPoDa kwa Mkoa wa Pwani Bi. Rehema Kawambwa akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi mara baada ya kuwatembelea katika maadhimisho ya Siku ya Ushairi wa Watoto Duniani Oktoba 07, 2023

Siku ya Ushairi wa Watoto Duniani (WoChiPoDa-World Children’s Poetry Day imeadhimishwa Oktoba 07, 2023 katika shule ya msingi Mkoani na shule ya msingi Kambarage zilizopo wilaya ya Kibaha mkoani Pwani ambapo dhima ya mwaka huu ikiwa ni mimea

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mratibu wa WoChiPoDa Mkoa wa Pwani Bi. Rehema Kawambwa amesema, lengo la siku hiyo ni kuimarisha ari na morali kwa watoto kupenda kutunga na kuandika mashairi pamoja na kuwajengea watoto hamasa ya kupenda kusoma vitabu.

“Siku hii inatukumbusha wazazi, walezi na walimu kuwahamasisha watoto wetu, kuamsha ari zao na kuwapa motisha zaidi katika kupenda kuandika na kusoma vitabu, kutunga na kughani mashairi” alisema Bi. Kawambwa

Matukio katika picha yakimuonesha Mratibu wa WoChiPoDa kwa Mkoa wa Pwani Bi. Rehema Kawambwa na wanafunzi wa shule za msingi za Mkoani na Kambarage zilizopo wilayani Kibaha mkoani Pwani wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Ushairi wa Watoto Duniani Oktoba 07, 2023

Siku hii huadhimishwa kila Jumamosi ya kwanza ya mwezi Oktoba kila mwaka na ilianzishwa mwaka 2014 na Bi. Gloria Gonsalves aishiye nchini Ujerumani lengo likiwa ni kuwapa watoto motisha, ari na morali ya kupenda kuandika, na kuwajaza upendo katika usomaji wa mashairi ili kuwajengea mazingira mazuri katika kujifunza mambo mbalimbali yanayowazunguka kwenye jamii zao kupitia uandishi, na usomaji wa mashairi na vitabu kwa ujumla.

Previous articleMAWAZIRI WAWEKWA KIKAANGONI _ MAGAZETINI LEO JUMAPILI OKTOBA 08/2023
Next articleWANANCHI MTWARA WAVUNJA MKUTANO MKUU KISA MWENYEKITI WA KIJIJI

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here