Home KITAIFA MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA MARAGARASI-ILUNDE-UVINZA KWA KIWANGO CHA LAMI KUKAMILIKA...

MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA MARAGARASI-ILUNDE-UVINZA KWA KIWANGO CHA LAMI KUKAMILIKA OKTOBA, 2023

Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Ngoko Mirumbe akieleza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Maragarasi-Ilunde-Uvinza (KM 51.1) kwa kiwango cha lami mbele ya waandishi wa habari waliotembelea mradi huo Aprili 19, 2023

 

 

Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Ngoko Mirumbe akieleza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Maragarasi-Ilunde-Uvinza (KM 51.1) kwa kiwango cha lami mbele ya waandishi wa habari waliotembelea mradi huo Aprili 19, 2023

Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imelenga kuhakikisha inaiunganisha mikoa yote nchini kwa barabara za lami jitihada ambazo zinajidhihirisha kwa uwepo wa miradi mingi ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ndani ya mkoa husika ili lengo hilo litimie na hatimaye kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji ili kuchangia uchumi wa mkoa husika na taifa kwa ujumla.

Mkoa wa Kigoma ni Mkoa ambao kwa asilimia chache bado haujanganishwa kwa barabara na mikoa jirani pamoja na mikoa mingine nchini lakini kwa uwepo wa miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa kwa kasi ndani ya mkoa huu, inaashiria kwamba ndani ya muda mchache sana kutoka sasa Mkoa wa Kigoma utakuwa umeshaunganishwa kwa miundombinu ya barabara.

Malengo na jitihada hizi, haziendi mbali na kauli za Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Ngoko Mirumbe akiongea na waandishi wa habari wakati wa kutembelea mradi wa ujenzi wa barabara ya Maragarasi-Ilunde-Uvinza yenye urefu wa 51.1 kwa kiwango cha lami ambapo amesema mradi huo umefikia asilimia 31 ya utekelezaji wake.

Mhandisi Mirumbe ameongeza kuwa, mradi wa Maragarasi-Ilunde-Uvinza ni sehemu ya barabara kutoka Kigoma-Uvinza-Maragarasi yenye urefu wa 212.

“Mradi wa Uvinza-Malagarasi (KM 51.1) ambao ni sehemu ya barabara kutoka Kigoma-Uvinza-Malagarasi ambao ni kilometa 212 huku kilometa 105 kutoka Kigoma hadi Uvinza zikiwa zimeshajengwa kwa kiwango lami tayari ambapo sasa hadi kuelekea Tabora zimesalia Kilometa 61 ambazo zote mkandarasi yuko site akiendelea na kazi” alisema Mhandisi Mirumbe

Kazi mbalimbali za ujenzi wa barabara ya Maragarasi-Ilunde-Uvinza (KM 51.1) kwa kiwango cha lami kama zilivyokutwa na mpiga picha wetu Aprili 19, 2023

Kuhusu utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi Mirumbe ameeleza kuwa unatarajiwa kukamilika tarehe 7 Oktoba, mwaka huu

Kuhusu manufaa ya mradi kwa jamii, kaimu meneja huyo amebainishi kuwa, mradi umeajiri wafanyakazi 216 kati yao wafanyakazi wageni wakiwa ni 21 pekee.

Kwa upande wake Kaimu Mhandisi Mkazi, Mhandisi Yusuf Karera amesema, hadi sasa kazi mbalimbali za utekelezaji wa mradi huo zimefanyika ikiwemo kujenga makaravati 22 huku makaravati madogo yakiwa ni 19 na makaravati matatu.

Kaimu Mhandisi Mkazi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Maragarasi-Ilunde-Uvinza (KM 51.1) kwa kiwango cha lami, Mhandisi Yusuf Karera akiongea na waandishi wa habari juu utekelezaji wa mradi huo unavyoendelea.

Mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami Maragarasi-Ilunde-Uvinza yenye urefu wa 51.1 unagharimu zaidi ya shilingi bilioni 62. Mradi huu unatekelezwa kupitia mkandarasi STECOL Cooperation chini ya mhandisi mshauri Norplan Tanzania Ltd.

Previous articleSERIKALI YATOA TAMKO VITA SUDAN, WATANZANIA KUREJESHWA NCHINI _MAGAZETINI LEO ALHAMISI APRILI 20/2023
Next articleKAIMU MENEJA WA TANROADS TABORA: MRADI WA BARABARA YA KAZILAMBWA-CHAGU KWA KIWANGO CHA LAMI KUWEZESHA USAFIRI NA USAFIRISHAJI KATI YA TANZANIA NA NCHI JIRANI

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here