Home KITAIFA MOROGORO KUJA NA MKAKATI WA KUKUZA PAMBA NA KOROSHO

MOROGORO KUJA NA MKAKATI WA KUKUZA PAMBA NA KOROSHO

MOROGORO KUJA NA MKAKATI WA KUKUZA PAMBA NA KOROSH

Mkuu wa mkoa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema serikali ya mkoa huo inakusudia kuanza kuhamasisha kilimo cha zao la korosho pamoja na zao la pamba hasa kwa wananchi ili kuimarisha uchumi pamoja na kuongeza pato katika mkoa.

Akitembelea maonesho ya 30 ya nanenane kanda ya mashariki amesema lengo la Mkoa wa Morogoro ni kutaka kuzalisha tani 20,000 hadi 30,000 ifikapo mwakani.

Kaimu meneja bodi ya korosho tawi la Morogoro Jafari Matata amesema, bado hamasa kwa wakulima ni ndogo hasa kwa zao la korosho hivyo bodi hiyo imeandaa mkakati wa kusogeza huduma ya ugani kwa wakulima hao.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya ununuzi wa pamba Vitus Lipagila amesema, tayari wameanza mikakati ya kutengeneza mikataba kati yao na wakulima .

Previous articleACT YAIBUA HOJA TATU KUPANDA BEI YA MAFUTA _ MAGAZETINI LEO JUMAPILI AGOSTI 06/2023
Next articleWAZIRI ULEGA AAHIDI SERIKALI KUBORESHA MACHINJIO YA MBALIZI

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here