Home KITAIFA MKATABA WA MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA LABAY-HAYDOM (KM 25) WASAINIWA

MKATABA WA MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA LABAY-HAYDOM (KM 25) WASAINIWA

 

HAYDOM-MBULU

 

Mkataba wa Mradi wa ujenzi wa barabara ya Labay-Haydom Km 25 umesainiwa rasmi jana, ikiwa na hatua muhimu ya kuelekea kuanza kwa ujenzi wa barabara hiyo muhimu kijamii na kiuchumi kwa Wananchi wa Wilaya ya Mbulu.

Zoezi la kusaini Mkataba huo, limefanyika jana Mei 19/2023  katika Uwanjwa wa Haydom wilayani Mbulu na kuhudhuriwa na Mheshimiwa Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi Injinia Godfrey Kasekenya, Viongozi wa Chama na Serikali pamoja na wananchi wakiongozwa na Mh.Mkuu wa Mkoa wa Manyara Komred Charles Makongoro Nyerere.

Ujenzi wa barabara hii ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, na Dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha Miundombinu ikiwa ni Njia ya Kuchochea Shughuli za Kiuchumi na Kurahisisha Huduma kwa Wananchi.

Akizungumza kwa Niaba ya Wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Mbunge wa Jimbo hilo Komred Flatei Massay amempongeza na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa uamuzi huo muhimu kwa faida ya wananchi wa Mbulu,na ameiomba Serikali isimamie mradi huo kwa ukaribu ili uweze kukamilika kwa wakati na kwa viwango.

Previous articleNAPE AWATANGAZIA KIAMA MATAPELI, WEZI MTANDAONI_ MAGAZETINI LEO JUMAMOSI MEI 20/2023
Next articleWANAFUNZI TUMIENI MICHEZO KUJIFUNZA UZALENDO

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here