Home KITAIFA FEMATA YAZINDUA KITAMBULISHO CHA KIDIJITALI KWA AJILI YA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI

FEMATA YAZINDUA KITAMBULISHO CHA KIDIJITALI KWA AJILI YA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI

Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji wadogo wa Madini Tanzania ( Femata ) imezindua semina ya uzinduzi wa mafunzo ya mradi wa vitambulisho vya Kidijitali kwa wachimbaji wa madini Tanzania lengo ikiwa kujua idadi ya wachimbaji wadogo ili kusaidia kuanzisha kanzidata.

Rais wa Shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa Madini Tanzania ( Femata ) John Bina amesema, vitambulisho vya wachimbaji wadogo wa madini kitawasaidia kuwatambua wachimbaji katika Taasisi za serikali ili waweze kukopesheka katika Benki kutokana na kutoaminika pia kutambulika katika uchimbaji sehemu yoyote ya Tanzania

Hivi vitambulisho tunafikilia kuvitumia katika uchaguzi na pia ndio iwe njia ya kupata wanachama na kwenye katiba moja ya vitu vilivyozungumzwa kuhakikisha Femata inatembea katika mstari mmoja hiki kitambulisho kinatolewa kuwa ni cha Femata lakini mwanachama awe amejiandikisha katika vyama vyao vya mikoa,John Bina” Mwenyekiti Femata.

Previous articleWAKALA WA MELI TANZANIA WAUNGA MKONO UJIO WA DP WORLD
Next articleMSITISHWE NA KUOGOPA MANENO//DP WORLD NI FURSA KWA WANANCHI-MBUNGE KEYSHA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here