Home KITAIFA DC BENO MALISA AZINDUA KITABU CHA KUZUIA NA KUKABILIANA NA UKATILI DHIDI...

DC BENO MALISA AZINDUA KITABU CHA KUZUIA NA KUKABILIANA NA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Mhe. Beno Malisa leo amezindua kitabu cha kuzuia na kukabiliana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto

Uzinduzi huo Umefanyika katika Hotel ya Eden jijini Mbeya chini ya taasisi inayoziunganisha taasisi za dini nchini TIP.

Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kukemea vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia katika jamii na kuhimiza juu maadili.

Aidha, ameipongeza TIP kwa jitihada za kuandaa kitabu hicho kinachokemea vitendo hivyo

Pia DC Malisa amepongeza mchango wa wadau kama vile UNICEF na UNFPA kwa kuwa, imara kupingana na vitendo vya unyanyasaji katika jamii.

DC Malisa amesisitiza wadau kupeleka elimu ya maadili shuleni na katika ngazi za familia ili jamii ipate kunufaika na elimu ya maadili.

Previous articleHATIMAYE NDOTO YA MTOTO HAMIMU YA KUKUTANA NA RAIS SAMIA YATIMIA
Next articleMKOA WA MWANZA WAADHIMISHA MIAKA 59 YA MUUNGANO KWA KUZINDUA KAMPENI YA UHIFADHI MAZINGIRA NA CHANJO

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here