Kanisa Assemblies of God TAG wafanya ibada ya kuliombe Taifa na Viongozi wake ikiwa ni siku ya kilele cha Siku ya wanaume Wakristo waumini wa Kanisa hilo ambapo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mh. Beno Malisa alishiriki ibada hiyo Na kuwasihi na kuwaomba kuiombea nchi yetu Tanzania baraka, utulivu na amani.
Aidha Dc Malisa amesema kuwa ili Taifa liweze kuongozwa vyema ni jukumu la kila Mmoja kuwaombea Viongozi wa Taifa hili ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan, wasaidizi wake, lakini pia kumuombea Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Juma Zuberi Homera na Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Dkt Tulia Ackson.
Ibada hiyo imeongozwa na Mchungaji wa Kanisa hilo Amnon Mwakitalu