Home KITAIFA DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUVIFANYA VIVUTIO VYA UTALII MWANZA NA MIKOA JIRANI KUFIKIKA...

DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUVIFANYA VIVUTIO VYA UTALII MWANZA NA MIKOA JIRANI KUFIKIKA KIRAHISI

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Adam Malima akiongea

 

 

Na mwandishi wetu, Sengerema

Kila mradi mmoja wa maendeleo unakuwa na athari katika eneo lingine. Ni kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Adam Malima akiongea na waandishi wa habari Aprili 23, 2023 mkoani Mwanza alipokuwa akielezea mradi wa ujenzi wa daraja la Kigongo-Busisi litakavyochochea uchumi na ukuaji wa sekta nyingine za kiuchumi ikiwemo sekta ya utalii.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Adam Malima akiongea na waandishi wa habari kuhusu mchango wa daraja la Kigongo-Busisi katika kukuza uchumi wa mkoa huo na sekta nyingine ikiwemo sekta ya utalii

Malima amesema daraja hilo litakapokamilika litatumika kama lango la utalii kwa kurahisisha usafiri wa kuvifikia vivutio vya utalii vya Mkoa wa Mwanza na mikoa jirani na hatimaye kuchangia pato la Taifa.

Picha tofauti zikionesha mwonekano wa daraja la Kigongo-Busisi ambazo ujenzi wake unaendelea

Kufuatia umuhimu huo, Malima ametoa onyo kwa baadhi ya watu ambao sio waaminifu wanaoiba vifaa vya miradi ya ujenzi.

“Kuna baadhi ya watu wanaona kuwa wanapoiba vifaa vya miradi ni kama wanamuibia mkandarasi kumbe wanamuibia Rais Samia pamoja na sisi Watanzania” alisema Malima na kuongeza

“Tukikuta duka linalouza vifaa vilivyoibwa kwenye miradi ya ujenzi tutalifunga, na mwenye duka huyo hatafanya tena biashara katika Mkoa wa Mwanza labda akatafute leseni mkoa mwingine na lazima atatueleza mnyororo wote”

Aidha, mkuu huyo wa mkoa ameahidi kutoa ushirikiano wa dhati katika nyanja zote kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kuhakikisha kwamba mradi huo unakamilika kwa wakati.

Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigongo-Busisi umeweza kutoa fursa za ajira 1,001 ambapo zaidi ya asilimia 94 ya walioajiriwa ni wazawa

 

Kazi mbalimbali za ujenzi wa daraja la Kigongo-Busisi zikiwa zinaendelea, ujenzi wa daraja hilo umefikia asilimia 72 na ujenzi unatarajiwa kukamilika tarehe 25 Februari, 2024

 

 

Previous articleNYONGEZA, KODI KILIO WATUMISHI_ MAGAZETINI LEO JUMATATU APRILI 24/2023
Next articleMENEJA WA TANROADS MWANZA: TANGU RAIS SAMIA AINGIE MADARAKANI KASI YA UTOAJI FEDHA KUHUDUMIA MIRADI IMEKUWA KUBWA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here