Home MICHEZO BULAYA CUP KUTIMUA VUMBI LEO

BULAYA CUP KUTIMUA VUMBI LEO

Mashindano ya Bulaya Cup yanatarajiwa kuanza kutimua Vumbi leo Oktoba Mosi,2023 katika viwanja mbalimbali wilayani Bunda mkoani Mara huku mashindano hayo yakishirikisha timu 22.

 

Mshindi wa kwanza wa mashindano haya ataibuka na kiasi cha shilingi Milioni 2 mshindi wa pili milioni 1 huku mshindi wa tatu atajinyakulia laki 5.

 

Akikabidhi jezi mwandaaji wa mashindano hayo Mbunge wa Viti Maalum Ester Bulaya amesema mashindano hayo yanalenga kwenda kuibua vipaji ambavyo viko katika wilaya kama ilivyo kawaida yake.

 

“Mashindano haya yamewaibua akina Sixtus Sabilo pamoja na kina majogoro ni wakati sasa wakuangalia vipaji vingine wameniomba nami nimeitika.

 

Mashindano hayo yatagusa michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa miguuu wanawake Mpira wa miguuu wanaume,Pete,Bao ,pooltable n.k huku Fedha ya mashindano yote ikigharimu kiasi cha shilingi Milioni 20

Previous articleGGML YATOA DARASA KWA RAI WA UGANDA JUU YA TEKNOLOJIA MPYA UCHIMBAJI MADINI
Next articleKUNENGE AKABIDHIWA RUNGU KUNYANG’ANYA VISIWA NA VIWANJA VILIVYONG’ANG’ANIWA NA WAWEKEZAJI BILA KUENDELEZWA KWA MUDA MREFU

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here