Home KITAIFA BANDARI HAIJAUZWA – MHE. KASEKENYA

BANDARI HAIJAUZWA – MHE. KASEKENYA

Mbunge wa Jimbo la Ileje na Naibu Waziri wa ujenzi na Uchukuzi Mhe. Godfrey Kasekenya Msongwe jana alifanya ziara katika kata ya Kalembo katika kijiji cha Mbangala na kufatiwa na mkutano wa hadhara uliyofanyika katika Kijiji cha Kalembo

Akiwa katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kalembo Mhe. Kasekenya aliweza kuzungumzia swala la bandari na kusema
“Bandari yetu haijauzwa ila kinachofanyika ni uwekezaji ambapo kwa sasa tunaingiza tirioni 6 kwa mwaka itapanda mpaka kuwa tirioni 26 kwa mwaka”

Mhe. Kasekenya pia alisikiliza kero za wananchi na kuzitolea ufafanuzi. Moja ya kero iliyowasilishwa ni kukosekana sehemu ya kulala ndugu ambao hupeleka wagonjwa katika hospital ya Wilaya ya Ileje

Akiwa katika Kijiji cha Mbangala Mhe. Kasekenya alikagua miundombinu ya shule na barabara pamoja na msingi wa ujenzi wa zahanati ya Kijiji inayojengwa na Wananchi na kuchangia shilingi laki 2

Ndugu. Jackson Mbuba mwenyekiti wa Tawi la CCM Mbangala alisema amefurahishwa na ujio wa mbunge na kumuomba alitazame swala la barabara kwani imekuwa changamoto kubwa katika Kijiji hicho

Previous articleDKT. MPANGO MGENI RASMI UFUNGUZI WA MAONYESHO YA NANENANE 2023 MBEYA
Next articleWAZIRI AMPA KIBANO CHA SIKU 15 MKANDARASI _ MAGAZETINI LEO JUMANNE AGOSTI 01/2023

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here