Home KITAIFA ALIYEMSHAMBULIA MTEJA BAADA YA KUSHINDWA KULIPA 500 ASAKWA NA POLISI

ALIYEMSHAMBULIA MTEJA BAADA YA KUSHINDWA KULIPA 500 ASAKWA NA POLISI

 

Mfanyabiashara Harid Njianguru,mkazi wa Kidatu Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro anasakwa na polisi kwa tuhuma za kumshambulia mteja wake na kusababishia madhara makubwa baada ya kushindwa  kulipa  kiingilio cha Sh 500 kuangalia mpira kati ya timu ya soka ya Azam FC na Tanzania Prisons kwenye ukumbi wa baa anayomiliki.

Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro Alex Mkama,amesema tukio hilo lilitokea usiku wa Agosti 28, 2023 katika kijiji cha Mkamba Wilaya ya Kilombero baada ya mfanyabiashara huyo kumshambulia Protas Komba (40) kwa kumpiga na kisha kumsukuma na kuangukia kisogo na kupoteza fahamu.

Amesema Komba alifika baa ya mfanyabiashara huyo ambayo inajulikana kwa jina la Kigamboni’ ili kuangalia mchezo huo na kwamba alishindwa kulipa kiingilio cha sh 500 na akawa analazimisha kuingia ndani ya baa.

Previous articleREA YATEKELEZA MRADI WA BIL 22, KUWANEEMESHA WANANCHI KWA KUKAMILISHA KITUO CHA KUPOZA UMEME IFAKARA
Next articleWANAOWEKA PICHA ZA KUDHALILISHA MITANDAONI WAONYWA.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here